Mbele yenu nimerudi, kuwauliza suali
Naitia na juhudi, ili munipe ukweli
Musizifanye kusudi, kunificha jambo hili
Muwekao pasiwadi, ni kipi munachoficha?
Hata wapenzi wa jadi, hawajaepuka hili
Wangafanya jitihadi, yawe mapenzi ya kweli
Ela kuna la wahedi, laitatiza akili
Muwekao pasiwadi, ni kipi munachoficha?
Mwakificha kitu gani, mbona munanitatiza
Munamfichia nani, ambae anawakwaza
Kwani muna siri gani, ni nani atanijuza
Muwekao pasiwadi, ni kipi munachoficha?
Hapa kambi naikita, siondoki asilani
Mukija mutanikuta, nimekaa mkekani
Kidevu mekifumbata, muneleze kwa makini
Muwekao pasiwadi, huwa munaficha nini?
*RUIYA SALIM*